Psalms 115:4-8


4 aLakini sanamu zao ni za fedha na dhahabu,
zilizotengenezwa kwa mikono ya wanadamu.

5 bZina vinywa, lakini haziwezi kusema,
zina macho, lakini haziwezi kuona;

6 zina masikio, lakini haziwezi kusikia,
zina pua, lakini haziwezi kunusa;

7 zina mikono, lakini haziwezi kupapasa,
zina miguu, lakini haziwezi kutembea;
wala koo zao haziwezi kutoa sauti.

8 cWale wanaozitengeneza watafanana nazo,
vivyo hivyo wale wote wanaozitumainia.

Copyright information for SwhKC